Misri (1805-1881)

Misri (1805-1881) ni kipindi katika historia ya nchi ya Misri ambako mabadiliko mengi yalitokea yaliyopelekea jinsi Misri ya leo ilivyo. Mabadiliko haya yalikuwa ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Kilikuwa ni kipindi cha mvuvuko wa nchi kutoka hali ya ukabaila kwenda katika uchumi wa kibepari. Ndani ya kipindi hiki Misri iliweza kujizatiti kutoka tawala za nje na hasa zile za Ulaya. Mifumo mbalimbali ya elimu ilianzishwa katika kipindi hiki. Pia mapinduzi ya nchi hii mnamo miaka ya 1881/1882 yalileta sura mpya katika nchi ya Misri hasa katika mtazamo wa dini ya kiislamu. Halikadhalika mapinduzi yalijaribu kuinasua nchi kutoka katika ukandamizaji wa Kiingereza kitendo ambacho hakikufanikiwa kwa kiwango cha juu.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search